Mamilioni ya wananchi wa Hindia wamekusanyika kusherehekea sherehe za Kimila

Bruno Kaitaba


 Umati mkubwa wa mahujaji wa Kihindu umekusanyika nchini India na kuoga katika maji wanayoamini kuwa matakatifu Jumatatu katika wa ufunguzi wa tamasha la ibada linalofahamika kama Kumbh Mel

Umati mkubwa wa mahujaji wa Kihindu umekusanyika nchini India na kuoga katika maji wanayoamini kuwa matakatifu Jumatatu katika wa ufunguzi wa tamasha la ibada linalofahamika kama Kumbh Mela.

Waandaaji wa  tamasha hilo wanatarajia watu milioni 400 watashiriki kwenye kusanyiko hilo kubwa zaidi kuwahi kutokea. 

Tamasha la kidini la Wahindu linalohusisha ibada ya kuoga linafanyika katika eneo inapokutana mito mitatu, Ganges, Yamuna na Saraswati.

 Waziri Mkuu wa India Narendra Modi ameliita kusanyiko hilo kuwa  "tukio takatifu" linalounganisha pamoja watu wengi katika imani, ibada na utamaduni. Naye Waziri kiongozi wa jimbo la Uttar Pradesh Yogi Adityanath, amewakaribisha mahujaji kwenye tamasha alililota kuwa kubwa zaidi la kiroho na kiutamaduni.

Wakati wa kuanza kwa tamasha hilo, watawa wa Kihindu wameonekana wakiwa wamebeba bendera kubwa za madhehebu yao wakati matrekta yakikokota sanamu za miungu ya kihindu na kusindikizwa na tembo. Mahujaji waliojitokeza kwa wingi wamesikika wakipiga ngoma pamoja na honi kama sehemu ya ibada yao.

Post a Comment

Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.