Moto waendelea Los Angeles







 


 Jimbo la Lose Angels nchini Marekani limeendelea kuteteketea kwa moto ambao ulizuka usiku wa kumkia januari 9 2025 huku ajali hiyo ikiendelea kusababisha vifo na kuharibu miundombinu


Taarifa ya mchunguzi wa kiafya wa jimbo hilo, imesema mpaka sasa vimeshatipotiwa vifo zaidi ya kumi na miili hiyo inasubiri kutambuliwa kisheria na ndugu zao.

 

Mapema jana, Rais Joe Biden alisema kuwa moto huo unaowaka katika eneo la Greater Los Angeles, ulikuwa mbaya zaidi kuwahi kushuhudiwa katika historia ya jimbo hilo la magharibi mwa Marekani. 


Biden amesema watu 360,000 wameondolewa hadi sasa. Hata hivyo, chanzo cha moto huo bado hakijajulikana. 


Maelfu watumwa kuukabili moto wa nyika Californiaulingana na Mkuu wa Kikosi cha Zimamoto cha Los Angeles, Kristin Crowley, zaidi ya nyumba 5,300 zimeharibiwa katika kitongoji cha Pacific Palisades peke yake tangu siku ya Jumanne. 


Aidha, Takribani majengo 4,000 hadi 5,000 yameungua au kuteketea kabisa katika eneo la Eaton Fire karibu na Pasadena.

Post a Comment

Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.