Wachimba Mgodi walio kuwa wamekwama wakwamuliwa

Bruno Kaitaba




Dakika 33 zilizopita

Zaidi ya wachimba migodi haramu 26 wameokolewa na karibu miili kumi kuondolewa kwenye mgodi uliotelekezwa nchini Afrika Kusini.

Operesheni za uokozi zilianza tena leo kuwafikia watu zaidi ambao huenda bado wamekwama mgodini humo.

 Kiongozi wa jamii ya eneo hilo, Johannes Qankase, amesema wachimba Mgodi waliookolewa ni wamedhoofika mno na wana upungufu wa maji mwilini.

Amesema wengi wao wamepelekwa hospitali wakati wawili wanaaminika kuwekwa kizuizini na polisi.

 Maafisa wa serikali wanatarajiwa kulitembelea leo eneo hilo la mgodi huku shughuli ya uokozi ikiendelea.


Operesheni hiyo inafuatia sakata ya wiki kadhaa kwenye mgodi huo uliotekelezwa, ambapo maafisa wanatuhumiwa kwa kujaribu kuwalazimisha wachimbaji hao kujitokeza nje kwa kuzuia chakula na maji kuteremshwa kwao na jamii ya eneo hilo.

Haijulikani wazi ni watu wangapi waliobaki kwenye mgodi huo. Serikali imesema jana kuwa zaidi ya watu 1,000 wanaohusika na uchimbaji haramu wa madini katika eneo hilo wametoka mgodini na kukamatwa mpaka sasa.

Post a Comment

Oops!
It seems there is something wrong with your internet connection. Please connect to the internet and start browsing again.
AdBlock Detected!
We have detected that you are using adblocking plugin in your browser.
The revenue we earn by the advertisements is used to manage this website, we request you to whitelist our website in your adblocking plugin.